Psalms 7:1-5

Sala Ya Mtu Anayedhulumiwa

(Ombolezo La Daudi Kwa Bwana Kwa Sababu Ya Kushi, Mbenyamini)


1 aEe Bwana, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe,
uniokoe na kunikomboa na wote wanaonifuatia,

2 bla sivyo watanirarua kama simba
na kunichana vipande vipande, asiwepo wa kuniokoa.


3 cEe Bwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya
na kuna hatia mikononi mwangu,

4 dau ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami,
au nimemnyang’anya adui yangu pasipo sababu,

5 ebasi adui anifuatie na kunipata,
auponde uhai wangu ardhini
na kunilaza mavumbini.

Copyright information for SwhKC